Posts

Showing posts from June, 2023

TATHMINI YA MJADALA KATIKA FORUM YA KATIBA YA WATU KUWEKA USAFI WA MAZINGIRA KAMA HAKI YA MSINGI KIKATIBA YA WATANZANIA

Image
I. Utangulizi T athmini kuhusu umuhimu wa kuweka msingi uliojengwa imara na kuweka mwelekeo wa kitaifa kuwa usafi wa mazingira ni haki ya msingi ya Watanzania.  Tathmini  hii inazingatia umuhimu wa hatua hii katika kuboresha utekelezaji wa sera na sheria za usafi wa mazingira, kuimarisha uwajibikaji, kukuza ushiriki wa wananchi, kukuza maendeleo ya jamii, na kuhakikisha afya bora kwa wananchi wote.   II. Hali ya Usafi wa Mazingira nchini Tanzania Hali ya usafi wa mazingira nchini Tanzania inakabiliwa na changamoto kadhaa. Baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na uchafuzi wa mazingira, uharibifu wa vyanzo vya maji, usimamizi hafifu wa taka, na upungufu wa huduma za maji safi na vyoo. Hali hii ina athari kubwa kwa afya ya umma na maendeleo ya jamii.   III. Umuhimu wa Kuweka Usafi wa Mazingira kama Haki ya Msingi 1.     Uwiano na viwango vya kimataifa: Kuweka usafi wa mazingira kuwa haki ya msingi ya Watanzania ni kutekeleza wajibu wa Tanzania kulingana na viwango vya kimataifa vilivyowekwa

UTARATIBU WA USAFI WA MAZINGIRA NAO UWEKWE KWENYE KATIBA?SWALI LA MDAU KWENYE FORUM YA KATIBA YA WATU

Image
  [05:23, 28/06/2023] A: Utaratibu wa usafi wa Mazingira nao uwekwe kwenye katiba? Nimekuwa nikitatizika sana na usafi wa mitaa yetu. Hakuna jitihada zozote zinazoongelewa kuhusu usafi wa mazingira yetu. Inasikitisha sana kwamba tupo na ngazi za uongozi kutoka kwenye mitaa lakini hakuna utashi wa kuhimiza watu kusafisha mazingira. Mitaa yote Dar es salaam haisafishwi kila wakati inatoa harufu mbaya. Utakuta Mwenyekiti wa mtaa yupo hawezi hata kuhimiza vijana wakachimbua hiyo mitaro na kusafisha mazingira.  Mfano: Dodoma maeneo ya Airport sehemu ambayo inamkusanyiko mkubwa wa watu Chako ni Chako mitaro inatoa harufu mbaya miezi yote 12.  Sababu za kutokea kwa jambo hilo Hakuna political will Hapa naongelea utashi wa kisiasa. Hakuna viongozi wenye utashi wa kisiasa maana hakuna mwongozo wa kuwaelekeza kuhamasisha watu kufanya usafi. Matokeo yake imekuwa ni tabia na watu wanaona hilo ni jambo la kawaida. Lazima kuwepo na miongozo kikatiba itakayoweka misingi ya usafi wa mazingira. Hii ita

KATIBA IJAYO IJIBU NINI JUU YA VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA? MDAU ALITUPA SWALI KATIKA MJADALA WA KATIBA YA WATU

Image
  MAJIBU Kabla hatuja pata majibu na mchakato wa katiba dhidi ya adui huyu na vita yake kikatiba, kwanza tujue hali ikoje na hadi sasa Taasisi tulizozipa mamlaka ya kusimamia zimetekeleza kwa kiwango gani na nini changamoto...nimefarijika baada ya hotuba ya Kamishina Jenelari  bwana Lyimo kwa kile alichokifanya ndani ya miezi mitatu ya uteule wake.. Tutaileta taarifa yake baada ya kuitolea tathimini na takwimu za utekelezaji alizofikia ndio twende mbele kujibu swali lako katika Katiba Ila ninacho jua........................................................ HALI DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA DUNIANI INA CHANGAMOTO KUBWA, NA BIASHARA HARAMU YA DAWA ZA KULEVYA BADO NI TATIZO LINALOENDELEA KUKUA.  Makampuni ya dawa za kulevya yanafanya kazi kwa njia mbalimbali na kujaribu kuepuka udhibiti wa kisheria na juhudi za kupambana na biashara hiyo.  Hii inaathiri hasa maeneo yenye umaskini mkubwa, migogoro ya kisiasa, na udhaifu wa mfumo wa sheria. Afrika ni moja ya maeneo yanayoathiriwa sana na tatizo