Posts

Showing posts from August, 2023

RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AMUAPISHA MKURUGENZI MKUU WA IDARA YA USALAMA WA TAIFA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Image
  Balozi mstaafu Ali Siwa amekuwa katika utumishi wa umma tangu mwaka 1977 na kuweza kushika nafasi mbalimbali za uongozi. Kati ya mwaka 2001 mpaka 2014, Balozi Mstaafu Ndugu Siwa alikuwa Afisa Mambo ya Nje, Mkuu katika ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Abu Dhabi iliyoko nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates); Moscow, nchini Urusi na baadaye Berlin, nchini Ujerumani. Mwaka 2014, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, alimteua Ndugu Ali Idi siwa kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kigali, nchini Rwanda, nafasi aliyoihudumu mpaka mwaka 2018 September 2018, aliteuliwa na Hayati Rais John Pombe Magufuli kuwa mwenyekiti wa bodi ya wadhamini NSSF, nafasi ambayo alikuwa anaitumikia mpaka mwaka 2023. . ​

MSAJILI AKUTANA NA VIONGOZI WA CHADEMA KUJADILI KUIMARISHA DEMOKRASIA NCHINI

Image
Mwenyekiti wa CHADEMA mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe (kushoto), akisisitiza jambo mbele ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, wakati wa kikao cha Msajili na viongozi waandamizi wa CHADEMA leo jijini Dar es Salaam. Kikao cha Msajili na CHADEMA ni juhudi za ofisi hiyo kuimarisha hali ya kisiasa hususan demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.  Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi (katikati) na viongozi waandamizi wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (kulia) wakimsikiliza Mwenyekiti wa CHADEMA, mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe (kwanza kushoto) wakati wa kikao cha Msajili na chama cha CHADEMA chenye lengo la kuimarisha demokrasia ya vyama vingi vya siasa kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe (kulia) akiteta jambo na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi (katikati), baada ya kumaliza kikao chenye lengo la kuimarisha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini

VIONGOZI PAMOJA NA BAADHI YA WANACHAMA WA CHAMA CHA WANASHERIA TANGANYIKA (TLS) PAMOJA NA CHAMA CHA WANASHERIA ZANZIBAR (ZLS) WAKIWA KWENYE KIKAO NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. SAMIA SULUHU HASSAN

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye Kikao na Wanachama wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) pamoja na Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZLS), Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 14 Agosti, 2023. Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Harold Sungusia akizungumza mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alipokwenda pamoja na ujumbe wake Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 14 Agosti, 2023. Rais wa Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZLS) Masoud Rukazibwa akizungumza mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati alipokwenda pamoja na ujumbe wake Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 14 Agosti, 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati alipokutana na Viongozi wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 14 Agosti, 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Rais wa

YALIYOJILI KATIKA HUKUMU YA KESI YA KUPINGA MKATABA WA UWEKEZAJI WA BANDARI 10 AUGUST 2023

Image
No 1 Majaji wote watatu wameingia muda huu saa 3:42. Majaji; Mhe. Ndunguru  Mhe. Ismail  Mhe. Kagomba Wakili wa serikali anatambulisha mawakili wa pande zote mbili. Na wote wako tayari kupokea hukumu. Mahakama imetulia kwa ukimya mkuu. Majaji wanazungumza kidogo, Mhe. Ismail na Ndunguru. Kisha, Jaji Kagomba na Ndunguru pia wanazungumza kidogo. Wanaendelea kuandika. Karani wa Mahakama leo ni MAPUNDA Majaji wanasema wako tayari kusoma hukumu na kwamba itasomwa kwa kiswahili Jaji Ndunguru: Kabla ya kuanza usililizwaji huo, Mawakili wa pande zote mbili waliunda kwanza viini vya kuamuliwa (Issues) pamoja na kiini kimoja ambacho kiliongezwa na Mahakama. Jaji Ndunguru: Wajibu Maombi wameeleza kwamba Bunge lilitoa taarifa kwa umma ili kupata maoni, na wamesema kwamba watu 72 walijitokeza kutoa maombi. Shauri hilo lilisikilizwa kwa njia ya mdomo, mawakili wa pande zote mbili wakiwakilisha wadaawa. Jaji Ndunguru anaanza kusoma hukumu. HUKUMU YA MAHAKAMA  Katika lalamiko hili waleta maombi wanne

KITUO CHA DEMOKRASIA TANZANIA (#TCD) MBIONI KUANZISHA JUKWAA LA WANAWAKE, KUTATUA CHANGAMOTO ZA SIASA NA UONGOZI.

Image
  KITUO cha Demokrasia Tanzania (TCD) kimefanya kikao na viongozi wa Jumuiya za wanawake wa vyama wanachama wa TCD kujadili namna ya kuanzisha jukwaa la wanawake chini ya Kituo hicho. Kikao hicho kimefanyika katika ofisi za Kituo cha Demokrasia Tanzania zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam leo Agosti 09, 2023 huku vyama; CHADEMA, CCM, CUF, ACT-WAZALENDO pamoja na NCCR - Mageuzi wakishiriki. CHAUMMA wameshiriki kuwakilisha vyama visivyo na wabunge/madiwani. Jukwaa hilo linaundwa ili kuwakutanisha pamoja viongozi wa Jumuiya za wanawake za vyama wanachama wa TCD kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kutatua changamoto za wanawake katika siasa na uongozi.

NI UPI WAJIBU WA SERIKALI YA TANZANIA KWA WANANCHI WAKE KIKATIBA? SWALI LA MDAU KATIKA MJADALA WA KATIBA YA WATU

Image
[10:41, 03/08/2023] A: Nimekuwa nawaza sana kuhusu katiba ya nchi ya kijamhuri. Kwamba inapoanza kuundwa huwa kuna misingi ipi inawekwa? Napenda kuuliza  Ni upi wajibu wa serikali ya Tanzania kwa wananchi wake kikatiba? Maana kwenye katiba yetu ya sasa hakuna sehemu imeeleza wajibu wa serikali wa moja kwa moja kwa wananchi. Ndio maana kuna mambo yanafanyika kwa utashi wa kiongozi tu na siyo kuongozwa na katiba.  Kulingana na katiba ya sasa serikali haina responsibilities zozote kwa wananchi, yaani inafanya mambo yote kama msaada tu, huku serikali ikiweka masharti magumu kwa wananchi na kuwabana walipe kodi. Yaani wananchi wanalazimishwa kulipa kodi huku serikali haina responsibility yoyote kikatiba [12:09, 03/08/2023] T: Mimi naanza kwa kwa maana ya maneno hayo mawili WAJIBU na SERIKALI kwanza [12:09, 03/08/2023] T: Neno "WAJIBU" linamaanisha majukumu au wajibu ambao mtu au taasisi inapaswa kutekeleza. Ni wajibu ambao mtu au kikundi hakiwezi kuepuka au kubadilisha. Wajibu huf

ACT -WAZALENDO ZANZIBAR YAFURAHISHWA ZOEZI LA UHAKIKI VYAMA VYA SIASA

Image
  Baadhi ya wataalam kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chama cha ACT – Wazalendo Zanzibar mara baada ya kumaliza zoezi la uhakiki wa chama hicho katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu zilizopo Vuga Mjini Magharibi.   Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa anayeshughulikia Uchaguzi na Ruzuku, Bi. Hollo Kazi (wapili kushoto) akisoma moja ya nyaraka za chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT – Wazalendo) wakati wa zoezi la uhakiki wa vyama vya siasa walipotembelea katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu Zanzibar zilizopo Vuga mkoa wa Mjii Magharibi Zanzibar  tarehe 09 Agosti, 2023. Wengine ni viongozi wa chama hicho Zanzibar na kushoto kwake ni Afisa Sheria toka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Bibi. Grace Mushi. Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa anayeshughulikia Uchaguzi na Ruzuku, Bi. Hollo akionyesha Ilani ya Uchaguzi ya chama cha Alliance for Change and transparency (ACT – Wazalendo)  mahususi kwa ajili ya upande wa SMZ wakati w

BARAZA LA VYAMA VYA SIASA TANZANIA LAJADILI HALI YA KISIASA NA UMUHIMU WA UMOJA NA AMANI

Image
  Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Ahmed Ally Akiteta j Mrajisi wa Asasi za Kirai Zanzibar, Mohamed  Abdallah  pamoja na mjumbe mwalikwa kutoka asasi ya kiraia YPC, Martine Mang’ong’o mara baada ya kumaliza Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam  tarehe 1 Agosti 2023. (Picha na: ORPP) Msajili wa Vyama vya Saisa, Jaji Francis Mutungi akiteta jambo na Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe mara baada ya kumaliza Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam  tarehe 1 Agosti 2023. Mwakilishi wa Chama cha NCCR Mageuzi, Joseph Selasini akichangia mada wakati wa Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam  tarehe 1 Agosti 2023. Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Zuberi