KITUO CHA DEMOKRASIA TANZANIA (#TCD) MBIONI KUANZISHA JUKWAA LA WANAWAKE, KUTATUA CHANGAMOTO ZA SIASA NA UONGOZI.

 






KITUO cha Demokrasia Tanzania (TCD) kimefanya kikao na viongozi wa Jumuiya za wanawake wa vyama wanachama wa TCD kujadili namna ya kuanzisha jukwaa la wanawake chini ya Kituo hicho.
Kikao hicho kimefanyika katika ofisi za Kituo cha Demokrasia Tanzania zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam leo Agosti 09, 2023 huku vyama; CHADEMA, CCM, CUF, ACT-WAZALENDO pamoja na NCCR - Mageuzi wakishiriki.
CHAUMMA wameshiriki kuwakilisha vyama visivyo na wabunge/madiwani.
Jukwaa hilo linaundwa ili kuwakutanisha pamoja viongozi wa Jumuiya za wanawake za vyama wanachama wa TCD kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kutatua changamoto za wanawake katika siasa na uongozi.

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya Vita vya Majimaji inaonesha kuwa awali walikamatwa machifu 48 na baadaye kukamatwa wengine ambapo idadi ya machifu walionyongwa na kuzikwa katika kaburi moja ilifikia 66.

UTARATIBU WA USAFI WA MAZINGIRA NAO UWEKWE KWENYE KATIBA?SWALI LA MDAU KWENYE FORUM YA KATIBA YA WATU

Mjadala kuhusu umuhimu wa elimu ya Katiba na uelewa wa sheria kwa wananchi unajumuisha masuala muhimu yanayohusu ujenzi wa demokrasia, utawala bora, na usawa katika jamii. Hapa kuna taarifa na tathmini ya kina juu ya mjadala huo: