Posts

Showing posts from September, 2022

UPI MSINGI WA KATIBA YA NCHI? LAZIMA IANZE NA NENO "SISI” TUMEAMUA ~ DR...

Image
Hii maana yake ni mamlaka ya wanachi kuamua ni namna gani wanapaswa waongozwe na Maisha Yao yaweje kwa hiyo Katiba sio suala la kupuuza na imetajwa kama msingi wa katiba ya sasa ya mwaka 1977 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania _________________________________________________________________ Sheria ya 1984 Na.15 ib.3 KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 1977 UTANGULIZI MISINGI YA KATIBA KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani: NA KWA KUWA misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu: KWA HIYO, BA

JAJI FRANCIS NYALALI AMBAYE ALIKUWA JAJI MKUU WA TANZANIA KWA MIAKA 23 KUANZIA MWAKA 1977 – 2000.

Image
Huyu ndiye jaji mkuu anayetajwa kuhudumu katika nafasi hiyo kwa muda mrefu kuliko wote nchini. Ni jaji mkuu anayetajwa kupata nafasi hiyo bila kuwa na muda mrefu katika nafasi ya jaji lakini aliitumikia kwa kipindi kirefu kwa ufanisi na mafanikio. Katika historia ya Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na Nyalali ndiyo viongozi waliotumikia nafasi zao za kuongoza mhimili wa dola kwa miaka 23 mfululizo. Wakati Nyalali akiwa jaji mkuu, Nyerere alikuwa Rais wa Tanzania kuanzia mwaka 1962 – 1985. Mnamo mwaka 1991, hatua za kwanza za mpito kuelekea kwenye  vyama vingi  zilianza wakati Mwinyi alipomteua  Jaji Mkuu Francis Nyalali  kuongoza tume ya kuchunguza kiasi cha umaarufu wa mfumo wa chama kimoja.  Tume hii iliwasilisha ripoti yao kwa Rais mnamo 1992, ikipendekeza kwamba serikali ibadilishe na nchi iwe na mfumo wa vyama vingi. Walitoa pendekezo hili licha ya ukweli kwamba ni asilimia ishirini na moja tu kati ya watanzania 36,299 walihojiwa walikubali mabadiliko haya.  Walakini, asilimia ham

MFUMO WA KISHERIA WA KUHUISHA MCHAKATO WA KUBADILISHA KATIBA “TUJISAHIHI...

Image
"Watu walio hatari sana ni wale ambao  wanafikiri  kuwa  wanajua  kila  kitu , wa l a hawana haja kujifunza zaidi. Hii ni tabia mbaya ambayo  huzuia  kabisa ma e ndeleo. Sababu moja ambayo ilitu z uia sisi Waafrika kuendelea ni majibu ya urahisi kwa matati zo makubwa ” TUJISAHIHISHE 1962 Mwal.Julius K.Nyerere

BAADHI YA WAZUNGUMZAJI WA MADA YA "MFUMO WA KISHERIA WA KUHUISHA MCHAKATO WA KUBADILISHA KATIBA" WAKIENDELEA KUTOA HOJA ZAO KWENYE KONGAMANO.

Image
Adv Analilea Nkya ' “Katiba lazima Itoe nafasi ya Uchaguzi kuwa huru na kufuata misingi ya democracy lakin kuhakikisha pia vyama vya siasa vinafanya kazi kwa ufasaha” Katiba yoyote lazima ianze na Neno "Sisi" Hii maana yake ni mamlaka ya wanachi kuamua ni namna gani wanapaswa waongozwe na Maisha Yao yaweje kwa hiyo Katiba sio suala la kupuusa ~ Dr Nshala Rugemeleza Adv Iddi Mandi ‘ Sheria ya kuandika katiba ilipaswa kuwa tofauti na Sheria nyingine ili kuweza kutoa nafasi kubwa ya ushiriki wa wananchi. Dr Elifuraha Laltaika." Lazima wote tushiriki katika upatikanaji wa Katiba Mpya.Kuwe na Hitaji la Katiba Mpya, Expert body ya kuchanganua mchakato wote, Mkutano maalam wa kikatiba ili kujua wapi pa kurekebisha, pia na Kura ya maamuzi"  

WADAU MBALIMBALI WAKIENDELEA KUTOA MAONI YAO JUU MCHAKATO WA KATIBA MPYA ULIOANDALIWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANGANYIKA, TAREHE 24,SEP 2022,JIJINI ARUSHA

Image
 

FUATILIA KONGAMANO LA KUJADILI NAMNA BORA YA KUHUISHA MCHAKATO WA KATIBA MPYA

Image
  Wadau mbali mbali wakifatilia kwa umakini mjadala wa kuhuisha mchakato unaohusu katiba mpya, mjadala huu unaendeshwa na taasisi ya kisheria @ TanganyikaLaw jijini Arusha.

KUSITISHWA KWA 'AFRIKANAIZESHENI' KULISABABISHA KUASI KWA JESHI LA TANGANYIKA MWAKA 1964

Image
SEHEMU YA PILI KAWAWA 'SIMBA WA VITA' JEMBE LA AFRIKANAIZESHENI Ili kuepusha shari, na ili Chama kisifarakane, Mwalimu akajiuzulu nafasi yake ya Uwaziri Mkuu wa Tanganyika Januari 16, 1962 ikiwa ni mwezi mmoja tu tangu Uhuru wa nchi mpya, na kuamua kurejea kijijini kuimarisha Chama kama Mwenyekiti wa Taifa wa TANU; na Rashid Kawawa akachukua nafasi ya Uwaziri Mkuu. Naye Oscar Kambona, ambaye wakati huo alikuwa Waziri wa Elimu, akawa Waziri wa Mambo ya Ndani badala ya Clement George Kahama. Wote wawili hao, Kawawa na Kambona wakaachiwa kazi ya kuwaondoa Wazungu katika vyeo walivyokuwa bado wanashikilia haraka bila visingizio. Akimteua Kawawa, Mwalimu alisema kwa hasira na kwa kuamrisha: “Tazama, Rashid, wewe ndiye Waziri Mkuu kuanzia sasa hivi. Shika kiti”. Na akijulisha mawaziri wake juu ya uamuzi huo, Mwalimu alisema: “Leo naacha kiti changu cha Waziri Mkuu. Kabla ya kujiuzulu, mimi mwenyewe nimechagua upya Baraza la Mawaziri, na Bwana Kawawa akiwa ndiye Waziri Mkuu na ninyi w

KUSITISHWA KWA 'AFRIKANAIZESHENI' KULISABABISHA KUASI KWA JESHI LA TANGANYIKA MWAKA 1964

Image
  SEHEMU YA KWANZA FUNGATE YA UHURU NA MADARAKA KWA WAZAWA USIKU wa kuamkia Januari 21, 1964, Jeshi la Tanganyika liliasi na kushikilia serikali kwa muda, tukio ambalo aliyekuwa Rais wa Tanganyika, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alilielezea kuwa ni “siku ya aibu sana kwa Taifa”. Wakati jeshi hilo likiasi; siku hiyo hiyo, na saa hiyo hiyo, majeshi ya Kenya na Uganda nayo yaliasi kwa staili hiyo hiyo. Maasi yote ya nchi tatu hizo yalizimwa na majeshi ya Uingereza siku moja na wakati huo huo. Kwa Tanganyika, maasi haya yalitokea wiki moja tu baada ya mapinduzi ya umwagaji damu ya Zanzibar, Januari 12, 1964. Disemba 9, 1961 Tanganyika ilipata Uhuru wake kutoka kwa Wakoloni wa Kiingereza, Mara baada ya Uhuru wake Tanganyika ilirithi karibu kila taasisi ya Umma iliyokuwa chini ya Serikali ya Kikoloni, likiwemo Jeshi kutoka kwa Wakoloni wa Kiingereza, Desemba 9, 1961, Jeshi hilo likijulikana kama “Kings African Rifles” – (K. A. R) na baadaye kuitwa “Tanganyika Rifles” (TR). Katika kipindi

Mwal Nyerere Akiwaaga Wanajeshi wa Kulinda Amani wa Nigeria Wanaoondoka ...

Image
Video isiyo na sauti za Rais Julius Nyerere wa Tanganyika akiwaenzi Maafisa na Wanaume wa Kikosi cha 3 cha Jeshi la Nigeria katika gwaride la kumuaga lililofanyika Ikulu jijini Dar-es-Salaam. Kikosi hicho, ambacho kiliongozwa na Luteni Kanali Yakubu Pam, kilikuwa kimechukua jukumu la polisi lililofanywa na makomando wa Wanamaji wa Kifalme wa Uingereza mwezi Aprili. Makomando wa Uingereza waliitwa na serikali ya Tanganyika baada ya jeshi la Tanganyika kufanya mapinduzi mwezi Januari. Jeshi la Nigeria lilipewa jukumu hilo baada ya mkutano wa dharura wa shirika la Umoja wa Afrika (OAU) mjini Dar-es-Salaam mwezi Februari. Wakati wa kazi hiyo, Luteni Kanali Pam alisimamia kazi za polisi pamoja na mafunzo. Tarehe 1 Septemba, askari 1,100 wa Jeshi jipya la Tanganyika walikamilisha programu ya mafunzo ya miezi mitatu. Wanajeshi hao, pamoja na askari wa kikosi cha 2 Tanganyikan Rifles walitarajiwa kufidia zaidi hasara ya Kikosi cha 1 ambacho kilisambaratishwa baada ya maasi. Nia ilikuwa kwam

BARAZA LA MAWAZIRI LA SERIKALI YA MADARAKA YA TANGANYIKA MARA BAADA YA BARAZA HILO KUAPISHWA JIJINI DAR ES SALAAM SEPTEMBA 3, 1960.

Image
Kutoka kushoto kwenda Kulia: Mstari wa Mbele Waliokaa: Chifu Abdullah Said Fundikira, Waziri wa Ardhi na Upimmaji, M J Davies, Waziri wa Habari, Julius K Nyerere, Waziri Kiongozi, Sir Richard Turnbull, Gavana wa Tanganyika, J S R Cole, Mwanashria Mkuu, Sir Ernest Vasey, Waziri wa Fedha, Derek N M Bryceson, Waziri wa Afya na Kazi. Mstari wa Nyuma waliokaa: Oscar Salathiel Kambona, Waziri wa Elimu, Paul Bomani, Waziri wa Kilimo na Maendeleo ya Ushirika, George Kahama, Waziri wa Mambo ya Ndani, Amir Habib Jamal, Waziri wa Mawasiliano, Nsilo Swai, Waziri wa Viwanda na Biashara, na Rashidi Mfaume Kawawa, Waziri wa Nyumba na Serikali za Mitaa. Kawawa na Kambona ndio waliopewa jukumu la Utekelezaji wa 'Afrikanaizesheni' mara baada ya kujiuzulu kwa Waziri Mkuu Nyerere.

HISTORIA INABAKI KUWA MWALIMU WA KILA JAMBO

Image
  Mstali wa Mbele kuanzia kushoto ni Salmin Amour,Ali Mzee Ali,Hassan Nassoro Moyo,Edward Moringe Sokoine,Aboud Jumbe,Juias Kambarage Nyerere,Rashidi Mfaume Kawawa,Cleopa Msuya na Kingunge Ngombale Mwiru, Mstari wa Nyuma ni Abdalla Said Natepe,Salimu Ahamed Salimu,Getruda Mongera,Seif Sharif Hamad, Paul Sozigwa,Daudi Mwakawago,Moses Nnauye na Alfred Tandau..Wazee wetu hawa walilitumikia Taifa hili wakati huo likiwa Changa kabisa