Posts

Showing posts from June, 2024
Image
   MAFANIKIO YA KIUCHUMI NA KIJAMII KUPITIA MIRADI YA SERIKALI NA TIC 2022-2024 Tanzania imepiga hatua kubwa katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa kipindi cha mwaka 2022 hadi 2024, kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC). Mchango wa Sekta ya Uvuvi  Sekta ya uvuvi inaendelea kutoa mchango mkubwa katika uchumi wa Tanzania, ikipunguza umasikini na kuimarisha usalama wa chakula na lishe bora. Uwekezaji unaofanywa na Serikali katika sekta hii unagusa maisha ya mamilioni ya wananchi, na kudumisha upatikanaji wa chakula chenye lishe.     Ujenzi wa Miundombinu Serikali imekamilisha ujenzi wa mzani wa kisasa Mikumi uliopo kwenye barabara kuu ya Morogoro - Iringa, pamoja na kuboresha mizani ya Mikese uelekeo wa barabara ya Dar - Morogoro. Hatua hizi zimefanikiwa kumaliza msongamano wa magari, hali inayochangia ufanisi katika usafirishaji na biashara.   Ongezeko la Mauzo ya Mbogamboga na Maua   Wakulima wa mbogamboga na maua wamenufaika san