MJADALA JUU YA KUMBUKUMBU YA MUUNDO WA KATIBA YETU NA NAMNA BORA YA KUWA NA MABADILIKO CHANYA YA KATIBA IJAYO UNAENDELEA


[15:18, 16/05/2023] G: Nadhani nchi kama nchi inahitaji ILANI YA TAIFA,achilia mbali za vyama vya siasa.Hili litasaidia kujipima na kupima Kila awamu tunayoipa dhamana.

Katiba mpya ni muhimu mno kwa kuwa kiuhalisia ina mapungufu kadhaa kama wengi walivyoainisha ila ninashauri kuwe na Ilani ya Taifa pia

[15:41, 16/05/2023] P: Excellent thinking...πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½πŸ‘πŸ½

[16:12, 16/05/2023] +255 68: Mawazo yangu ni bora tukawa jamhuri ya muungano kama ilivyo sasa ingawa maboresho ya katiba yanahitajika sana kwa mustaksbali was taifa letu

[16:20, 16/05/2023] T: Walioukwamisha mchakato ule ni wanasiasa..na ndio maana Rais Samia suluhu Hassan akamtaka Msajili akutane nao waliotukwamisha kwa ummoja wao na mlezi wao..kuyajadili kwa mapana mapendekezo ya kamati na kukubaliana kwa dhamira njema namna ya kuendelea na mchakato kwa ustawi wa Taifa letu..hapa sasa ni nia njema kama muhimili wa yote na sisi tukasema wakati haya yakisubiliwa Tujikumbushe na tuone kwa kiwango gani wanasiasa watajongea na hiyo nia njema....kwa maaana hiyo tiunaendelea piakuyaona kwa ufupi yaliyomo hadi tutafika yaliyojadiliwa na kupendekezwa na kuishia njiani 2015

[16:33, 16/05/2023] +255 68: Mama kafanya jambo kubwa na huenda kaona mbali sana

[16:35, 16/05/2023] K: hapa umejibu swali la wengi la "tulifeli" wapi...maana isipokuwa tumekubaliana ; MOSI kwamba tulifeli na PILI sababu ya kufeli tutapata shida kukubaliana kwamba TUNAPOANZA UPYA nini tukwepe na wapi tusiende na kwa vipi tukubaliane kutokubaliana maana ni ukweli usiopingika kuwa hatufurahishana kwa asilimia 100 katika mchakato huu hii ni KANUNI ya ubinadamu hivyo basi naunga mkono hoja kwa kuzingatia Historia twende PAMOJA na TUFUNGUKE

[16:50, 16/05/2023] K: Nataka KUAMINI kwamba hatuta "reinvent the wheel" kwenye mchakato huu, tayari KATIBA TUNAYO ila mchakato uliofeli Ulijaribu kupata maoni ya Wananchi na kuchakata na Bunge maalum likaanza Kujadili, wakati wa Mjadala kundi moja la wadau likakasirishwa na jambo wakatoka katika mjadala na hili likatia dosari mchakato mzima; pamoja na kwamba uliendelea na kufikishwa "mwisho" LEO Mh. Rais ameona kuna umuhimu wa kurejelea hili jambo na labda Yeye awe wa kuweka Historia ya Pili (a record) ya kulileta Taifa Pamoja kwa Katiba Mpya yenye Ridhaa ya Asilimia Kubwa ya wananchi *bila ya shinikizo la wanasiasa

[18:14, 16/05/2023] T: ILANI YA TAIFA ni mpango wa muda mrefu ulioundwa na serikali ya kitaifa au chama cha kisiasa ili kufafanua sera za maendeleo ya nchi na kuainisha vipaumbele vya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Mpango huu unalenga kuleta maendeleo endelevu kwa taifa na kuweka msingi wa utekelezaji wa sera na mipango mingine mbalimbali ya serikali.                                                            

Baadhi ya mifano ya ILANI YA TAIFA ni pamoja na mipango ya maendeleo kama vile Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Tanzania (TDSP), Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUKUTA) na Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Zanzibar (PZDP II). Ilani hizi zinalenga kuleta maendeleo ya kiuchumi, kuondoa umaskini, kuimarisha huduma za jamii, kuboresha miundombinu, kukuza ajira na kuleta ustawi wa wananchi kwa ujumla. Sasa hapa sasa ndio 

Najaribu tu kutafakari juu ya

Uwajibikaji

Uadilifu

Usawa

Uwazi na Uhuru katika kufanya kazi


[18:17, 16/05/2023] K: Kipo Kitabu kimoja cha Dini kinasema nanukuu "misingi ikiharibika mwenye haki atafanya nini?" mwisho wa kunukuu       Namna au aina ya Msingi inaashiria "uzito" au ukuu wa mjengo(structure) inayelekea kujengwa. Hapa ninatamani sana tutumie nguvu nyingi kupaweka pawe BORA na Imara tukiwa tunakumbuka MAONO ya TANZANIA YA miaka 200 ijayo.🫑  I submit

[18:20, 16/05/2023] K: NI NINI MAONO YA TAIFA LETU tafakuri cho;onozi πŸ€”

[18:21, 16/05/2023] T: Ilani ya taifa ni mpango wa maendeleo wa kitaifa ambao unalenga kuelezea maono, malengo, na mikakati ya maendeleo ya nchi kwa kipindi cha miaka kadhaa ijayo. Ilani hii inaandaliwa na serikali ya nchi, na huwa inashirikisha maoni ya wadau mbalimbali wa maendeleo ya nchi kama vile wananchi, taasisi za utafiti, na wadau wa maendeleo.

Ilani ya chama, kwa upande mwingine, ni mpango wa maendeleo wa kisiasa ambao unalenga kuelezea sera, malengo, na mikakati ya chama cha siasa kwa kipindi cha miaka kadhaa ijayo. Ilani hii inaandaliwa na chama cha siasa, na huwa inashirikisha maoni ya wajumbe wa chama, viongozi wa chama, na wadau wa masuala ya siasa kwa ujumla.

[18:23, 16/05/2023] Tandawili : nilikuwa na jaribu kuona touti kati ya yale mdau aliyoyaona kwa umbali kuwa na Ilani ya Taifa

[18:24, 16/05/2023] K: ILANI yaani MANIFESTO?

[18:25, 16/05/2023] T: Maono ya Taifa letu Tanzania yanajumuisha kuwa na Taifa lililoendelea kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiutamaduni. Tanzania inatarajia kuwa na uchumi imara unaotokana na sekta zote za uchumi pamoja na kutumia rasilimali zilizopo kwa ufanisi mkubwa. Pia, Tanzania inalenga kuwa na jamii yenye usawa, yenye afya bora na elimu bora kwa kila mtu. Mbali na hayo, Tanzania inajitahidi kuwa na utamaduni imara, kuhifadhi mazingira na kufanya kazi na mataifa mengine kwa amani na ushirikiano.


[18:35, 16/05/2023] S: Ni kweli kabisa. Ila zipo doc nyingi sana zinazosimamia maendeleo ya Taifa. Ilani za vyama ni framework inayo compliment yale yaliyojadiliwa na wataalamu na kupitishwa kwenye vikao vyote kisheria ikiwemo Bunge na Baraza la Mawaziri. Mfano Vision 2025, MKURABITA, MKUKUTA, Mpango wa tatu wa Maendeleo wa Taifa (5 yrs) uliopitishwa miezi kadhaa iliyopita nk

[18:41, 16/05/2023] K: Katika Mahesabu kuna kitu kinaitwa Critical Path ….hii semi inatumika pia katika project management  maono ndiyo yanazaa DIRA na dira inazaa MALENGO ,..... critical path yetu kwa KATIBA ni Maono ya Nchi yetu

[18:51, 16/05/2023] K: Ilani (MANIFESTO) ni tamko la kina la sera(policies), malengo(GOALS) na vipaumbele(PRIORITIES) kwa taifa na wananchi wake kwa ujumla



[19:24, 16/05/2023] T: @P  alijaribu kutupitisha kimataifa kule juu kwamba athari za kiuchumi, kisiasa na kiusalama juu ya theory hii ya separation of power  katika nchi dhidi ya nchi zingine? Tafadhali kama kuna mdau anaweza kunifumbua zaidi itanisaidia kuwa balozi mzuri kwa wengi ninao wafahzmu.. si9jaona jibu la hii na ukiiangalia katiba yetu

[19:25, 16/05/2023] P: Hii approach imekuwepo kwa miaka sasa. Na sioni kama inatupeleka tunapotaka kwenda kwa speed inayoendana na upotevu wa rasilimali za nchi. Yaani the time it takes to achieve something plus the resources used to achieve that goal, is less or equal to neglegible!

Putting it bluntly, 'Serikali' ina upungufu mkubwa sana wa 'quality human resources'  yenye 'high quality skills set' wenye kiwango cha ubunifu wa karne ya kiushindani ya 21.

Kwa approach ya sasa ya serikali kuendelea kuandaa mipango ya maendeleo kwa kukusanya vi maoni vya hapa na pale (sijui toka kwa nani, mwenye uelewa na uzoefu toka wapi, God knows) tutaendelea kupata matokeo yale yale huku resources za nchi ziendelea kuwa expended.

We need a different approach. We need specified time and resour…

[19:34, 16/05/2023] P: @P leo umeswich on ! Unelectable hoja tunduizi a forward thinking approach kuleta solutions/suluhishi endelevu za vizazi vya kitanzania #200yearsthinking πŸ€”

[19:45, 16/05/2023] A: Nimesoma kila neno, haya ni mawazo chanya na yenye nia na maono ya kusonga mbele bila kujali vikwazo duni.

[19:56, 16/05/2023] T: huwa nafarijika sana na kuongeza maarifa mno nikisomaga vituvyako walah nasoma neno kwa neno halafu kwa sauti tukifika kwenye ile ya  Warioba tutatambua haya mambo yalipangwaje

[19:59, 16/05/2023] T: huyu atafutiwe nondo wadau

[20:02, 16/05/2023] A: Theory hii ya “separation of power” ina athari kubwa za kiuchumi, kisiasa, na kiusalama. 

Kiuchumi, inawezesha uchumi kukua kwa kuweka mamlaka tofauti katika mikono tofauti, kwa mfano, serikali inaweza kuweka sheria zinazohusiana na uchumi wakati bunge linahusika na bajeti za serikali. 

Kwa upande wa kisiasa, kuwa na mamlaka tofauti kunaweza kusaidia kuepusha madaraka yote kukusanyika katika mikono ya watu wachache. Hii inaweza kusaidia kuzuia ufisadi na kutokuwepo kwa utawala wa kiimla. 

Kiusalama, theory hii inaweza kusaidia kudhibiti vitendo vya ukandamizaji wa kisiasa na ukiukwaji wa haki za binadamu kwa kuweka mamlaka tofauti na madaraka

[20:37, 16/05/2023] A: Nimesoma Comment yako hii mpaka mwili wangu umesisimka

Nakumbuka mwalimu wangu katika somo moja kwenye topic ya 

THE ESSENTIAL AND MOST CRITICAL FACTORS FOR NATIONAL DEVELOPMENT

Kuna msingi na nguzo zinazojenga taifa. Kisha mambo mengine yawekwa 

Foundation (Msingi)

1. Patriotic and Ethical Leadership at all levels

2. National Unity of Purpose everyone and all resources dedicated to building one “ NATION HOME

3. Strategic Resources - People, Natural Resources and Financial Resources 

Pillars (Nguzo)

1. Production - Agriculture, Livestock, Fisheries, Forestry, Mining; Industrial Manufacturing 

2. Commerce - Trade, Tourism, Financial Services ( Banking, Insurance, Brokerage ), Media, Marketing,

3. Infrastructure Economic and Social Services; 

4.Institutions - Academia, Political Parties, Legislature, Judicial System Courts Statutory and Traditional Community systems of Justice ) Government, Business, Organized Labour, Faith Based Organizations

[20:50, 16/05/2023] A: Huwa inanishangaza sana watu wanapoenda kwenye nyumba za ibada hawalazimishwi na mtu kutoa sadaka na fungu la kumi. 

Lakini watu wanakuwa waaminifu sana, hii ni kutokana na kwamba wahubiriwa Ideology na wameielewa vizuri sana.

The nation which does not its own Ideology ni kama kipofu anatembea kwenye taa na hajui anapoelekea.

Tukiwa na Ideology as a Nation kila kitu tutakijenga juu yake. Plans, Ethics na vitu vingine vitajengwa kutokana na Idelogy yetu

Kwenye katiba ya sasa imeelezwa Tanzania ni nchi ya Kijamaa inaendeshwa na vyama vingi. Lakini ujamaa wenyewe hatujaueleza ni ujamaa upi huo?

Lazima tueleze ujamaa wetu ipoje kila mtu aujue.

[20:52, 16/05/2023] Asia Mohamed: TUME YA KUDUMU YA MIPANGO, UCHUMI, NA MAENDELEO YA TAIFA ina jukumu la kutekeleza mipango ya maendeleo ya miaka mitano katika nchi ya Tanzania. Tume hii inajumuisha wataalamu wa uchumi, sera na mipango ya maendeleo. Baadhi ya majukumu ya Tume hii ni pamoja na:

Kukusanya, kuchambua na kutoa taarifa za kiuchumi, kijamii na kimazingira

Kukusanya na kuchambua data za kiuchumi na kijamii na kuandaa mipango ya maendeleo ya taifa

Kutoa miongozo na ushauri kwa serikali na taasisi nyingine kuhusu sera na mipango ya maendeleo ya taifa

Kusimamia utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya taifa na kutoa tathmini ya utekelezaji wake. Tujivunie Kuwa Watanzania tuendeleze uzalendo katika kuhakikisha Tunaijenga Nchi yetu kwa maarifa na nguvu zetu zoteπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡Ώ

[20:55, 16/05/2023] K: Maono….Vision….ya Taifa la Tanzania ni kuwa Taifa lililoendelea kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiutamaduni.

πŸ‘†πŸ»Wadau mnaonaje hii kama Maono(Vision)

Hili tamko la maono Haitakiwi kuwa mambo mengi, maana ndiyo inatutengenezea  Dira na Malengo ya muda mfupi na Mrefu.

Halafu sasa ndipo tunaiweka Katiba ituratibu kufikia maono haya

MJADALA UNAENDELEA....

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya utawala wa Kijerumani katika eneo la Tanganyika inahusisha kipindi cha ukoloni wa Kijerumani ambacho kilidumu kati ya mwaka 1885 na 1916