MJADALA JUU YA NAMNA BORA YA KUWA NA KATIBA MPYA,UELEWA WA MCHAKATO MZIMA NA KUFAHAMU KATIBA YA SASA UNAENDELEA KATIKA FORUM YETU YA KATIBA YA WATU MASWALI YA PAPO KWA HAPO YAMEULIZWA NA KUJADILIWA


[12:07, 11/05/2023] P: 

Ndugu zangu, 

Uzalendo wa kweli huwa haufundishwi darasani kwenye makongamano, warsha, au semina.


Uzalendo wa kweli hufundishwa na Serikali/nchi kuwafanyia wananchi wake vitendo chanya vyenye kuwawekea mazingira sahihi na bora ya kujitegemea na kufikia ndoto zao ndani na nje ya mipaka ya nchi yao.


Mimi sijawahi kufundishwa uzalendo na mtu darasani au mtaani.


Lakini mtu akihoji uzalendo wangu kwa nchi yangu niko tayari kumtoa roho!


Mimi nilijikuta NAIPENDA NCHI yangu na NIKO TAYARI kuipigania, kuilinda, na kuitumikia kwa moyo wangu wote na hata kwa uhai wangu...kutokana na jinsi serikali/nchi yangu ilivyonionesha upendo, kunijali, kunilinda, kunitetea, na kuniwekea mazingira wezeshi ya kuja kuwa hivi nilivyo 


[12:23, 11/05/2023] +: Hili neno UZALENDO nadhani linapaswa kutafsiriwa kwa upana once and for all. Tunapaswa tulijue kwa upya na katika tafsiri pana zaidi. Watanzania waliowengi, hasa wenye madaraka wanapaswa ku "unlearn and relearn" maana sahihi ya neno UZALENDO ikibidi liwe defined kwenye katiba.

Why? Kwasababu neno uzalendo lilitumika vibaya sana regime iliyopita na kuumiza watu wengi. Kila aliyehoji chochote kama raia huru alikuwa branded kuwa siyo mzalendo, na wengi walipata "taabu sana"


[12:26, 11/05/2023] T: Tutajadili kwa mapana kila jambo hapa lakini mjumbe mwenzetu alikuja hapa na hoja hii na huko nje wadau wa mlezi wanamlalamikia mlezi wao yaani msajili..hoja hii haijaisha..na Msajli yuko hapa...


[12:36, 11/05/2023] P: 

Huenda hata Msajiri akawa hajui maana halisi ya "uzalendo" kwa nchi.


Tusipuuze hili nalo neno..πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡Ώ✅

[12:59, 11/05/2023] Pr:

 Naomba niulize wawezeshaji wa hili jukwaa : je mchakato huu tunaanza upya kana kwamba uliositishwa haukuleta mambo yaliyokubalika ? Tutawajibikaje na Rasilmali iliyowekezwa kwenye mchakato uliyositishwa dakika za mwisho kwa sababu za kisiasa a a??? Kama kuna mambo ambayo hayakuwa na utata hayawezi kubebwa ili mchakato huu usimbebeshe mlipa kodi mzigo wa ziada? Naomba mwongozo🀷🏽‍♂️

[13:07, 11/05/2023] T: 

Hii ni Mada mpya kutoka kwa Mdau..Tunaweza kuendelea nayo tukisubili Nondo za Ofisi ya Msajili? wajumbe mnasemaje? Lakini kwa kifupi Hali ya uelewa wa hili jambo Tangu 2014 ni ndogo mno ukizingatia Vijana wetu wa sasa ambao kwa maelfu walikuwa wadogo kudadavua mambo yale,sasa jukumu kubwa kama wadau ni kujadili kwa mapana hapa na kuwaelimisha wengine juu ya Historia yote ya michakato ya Katiba Yetu na mustakabali wa baadae..wakati jukumu hili la uratibu liko kwa Msajili..wajumbe walipendekeza awali tumjue kwanza Msajili na ofisi yake na majukumu yake..wengi hawajui..hapo ndio tulianzia jana..Prof.


[13:28, 11/05/2023] Dr.: 

Asante! Baada ya kujua maana ya Katiba tungepata pia historia ya Katiba ya nchi yetu.

[13:36, 11/05/2023] Dr.: 

Wawezeshaji, naomba kama inawezekana tuwe na muda maalum wa kujadili kila mada. Mfano maana ya Ijue Katiba tujadili kwa siku mbili au tatu. Pia wajumbe wa hili group tuhimizane kutenga muda wa kufuatilia mijadala ya Katiba ndani na nje group πŸ™


[13:36, 11/05/2023] A: 

Nimepitia mada hii vizuri sana na nimeptia kipenegere kwa kipengere. 

Nadhani inatupidi tuanze kutazama Katiba kwa mtazamo mwingine. Badala ya kuwaza kitu cha kwanza kuhusu utawala, tuanze kuwanza kuhusu "How to manage our resourse". Kwa mtazamo wangu msingi wa kwanza ni kuongelea Management of our resource. 


Tuanze kuongelea kwanza our National Interest, Kwamba maslahi yapi ya Taifa letu tunataka tuyalinde baada ya hapo ndipo tuweze kuanza kuongelea Utawala, Haki na wajibu.


NB: wazo langu ni kwamba tuanze kwanza na "Management of Our Resources and Defining of our National Interest"


[13:38, 11/05/2023] K: 

Ikiwa kuna matumizi mabaya/yasiyo ya lazima  n.k n.k n.k 

Je tufanye Kesi kwanza? Au Tuchukue yatokanayo yanayofaa ili yatumike kwenda mbele kwa ubora? Au tusubiri tuwakamate waliotumia fursa vibaya kwanza…..choices…choices! 🀷🏾‍♂️


[13:45, 11/05/2023] M: Lisu na Silaha wakilalamika kuwa Rais anaonekana kuuteka mchakato wa Katiba na kuuweka mikoni mwa wale wale. Sijui walitaka afanye nini!! Rais kama taasisi vipo, vyombo chini yake vya kumsaidia kuhahakisha kuwa Katiba inayokusudiwa, inapatikana na kuridhiwa na Watanzania kwa ujumla wao. Hivyo naamini Msajiri wa Vyama vya Siasa ndiye mtekelezaji mkuu wa mchakato huu. Nadhani tusubiri kuona hatua atakazochukua kutekeleza jukumu hili.



[13:52, 11/05/2023] T: Ndio maana akamleta Msajili kama mlezi wao aongoze jahazi walitaka aanzie wapi?


[13:53, 11/05/2023] A: 

1. Kwanza kabla ya kuanza kuongelea utawala. Nimuhimu kuongelea Lengo letu sisi kama watanzania kuwa pamoja (The purpose  of Nationa)


2. Foundations of our nation. Je, Taifa letu lina misingi ipi?  (Philosophical, Moral, Cultural) Hii ndiyo misingi.


3. What is our national interest (Sisi kama Taifa maslahi yetu ni yapi. Kutokana na maslahi yetu tunataka tujenge taifa la namna gani?)


3. Lazima tuangalie hustoria yetu. Yaani tunataka Tanzania ya sasa lakini ni vizuri kuikubali historia yetu. 


ALL NATIONS HAVE FUNDAMENTAL INTERESTS THAT THEY WOULD LIKE TO DEFEND AND PRESERVE


[13:55, 11/05/2023] T: 

Muda tutaupanga sisi hapa nashauri kwa vile kunauchambuzi kwa sauti pia ni vema wadau kuwe na mpangilio kwa kifupi Tumeanza vyema na sasa tuweke bayana nini tunapaswa kukiweka awali HISTORY KWANZA



[13:57, 11/05/2023] P: 

Kwa vile Mwenzeshaji ameshauri tuairishe hii mada basi ngoja nisubiri wakati Mwafaka. Kwa ufafanuzi wangu nilieibua hii mada niseme tu kwamba kwa vile katiba ni Sheria mama/Sheria kuu inayobainisha misingi mikuu inayoelekeza  mamlaka  na mipaka ya wenye dhamana ya kuongoza na kubainisha haki za raia na wajibu wao pamoja na misingi ya uwajibikaji, basi bila Shaka mchakato uliyositishwa kulikuwa na misingi ambayo haikuwa na utata🀷🏽‍♂️je hatuwezi kuibeba? Hilo ni swali kuhusu mchakato🀷🏽‍♂️



[14:07, 11/05/2023] P:

 Hii ya kuanza kuelimishana kuhusu Katiba Mpya ni tactical maneuvre ya irresponsible stakeholders kuchukua hatua stahiki kumaliza hii deadlock.


Kwani tunataka wananchi waelimishwe juu ya Katiba kwani wao ndio waliokwamisha mchakato kukamilika?


Kama wananchi walizungukiwa nchi nzima wakatoa hadi maoni yao juu ya Katiba Mpya kweli walikuwa hajui wanachokifanya?


Unajua kuna vitu vinfanywa mpaka unacheka.


We are an independent nation of more than 60 years. Lakini kuna vitu tunafanya kama watoto wa miaka 6.


We wasted taxpayers money on a sham exercise. We should be ashemed and apologize to the public. 


Badala yake tunataka kuwarudia waliokwisha kutupa maoni yao juu ya Katiba kuwaelimisha nini?


How absurd..

[14:10, 11/05/2023] P: 

Watu wengi kina nani? Kwani hao watu wengi wasioelewa huwa tunasubiri waelewe kwenye mambo mengine yote yanayoamriwa bila uelewa au consent yao?



The rest is same old staff that have gotten this nation into this s**t

[14:42, 11/05/2023] M: 

Tusiyumbishane bure hapa. Ushiriki wa watu kwenye jambo lolote lile kote duniani, ni kupitia uwakilishi. Ndio maana tuna vyama vya siasa wanaowasilisha itikadi za vyama vyao kwa umma, na wabunge katika ngazi ya kuisimamia serikali na kutunga sheria. Hivyo mtu kusema watu wengi waelewe kwanza ndipo hatua zaidi zifuate, huo uwingi unaupima vipi kama sio kwa njia za kiuwakilishi zilizopo kufutana na Katiba na sheria za nchi! Group hii ni uwanja wetu kuchangia kile mtu anachokiona kingefaa kuzingatiwa au kuangaliwa katika mchakato huu wa sasa wa kutupatia Katiba itakayoridhiwa na umma wa Watanzania kupitia uwakilishi kwa njia moja au nyingine. Tushiriki kutoa mawazo/maoni humu ambayo naamini wahusika watayatumia katika ngazi zao za uwakilishi.


[14:47, 11/05/2023] T: 

Kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2022 Ongezeko la watotoni Mil 16 baada ya miaka 10 wengi wao watakuwa watu Wazima Rudi nyuma sensa ya 2012 mwaka mmoja baada ya mchakato kuanza..watoto wale ambao ni more than 40% ya raia wote leo ni watu wazima wala hawakuhusika kabisaa na hayo maoni na ndio kizazi kina hoji nini kilitokea


[14:49, 11/05/2023] T: 

Na ndio maana hata wewe leo huelewi kwanini Msajili anajukumu hili leo...


[14:51, 11/05/2023] P: 

Ufikiri wa aina hii ni very mediocre. Tukianza kusubiriana kila mtu ashikishwe basi hata hii Katiba iliyodumu kwa mingo zaidi ya 4 sasa ni uhalifu kwa wale ambao hawakushirikishwa?



[14:57, 11/05/2023] T: 

Ndio maana uko hapa kujadili namna bora ya kupata katiba bora kama Rais alivyoainisha na kumtaka Msajili kutekeleza jukumu la msingi kuwaita washirika wake wakuu vyama vya siasa wewe na walioleta mada wakataka kujua nini wajibu na jukumu la msajili katika hili Tuendelee kutoka hapo


[15:00, 11/05/2023] P: 

Nina hofu wadau wenzangu kuhusu mchakato wa Katiba ya Wote kuendesha na vyama vya siasa.vyama hivi ni wadau wanaowakilisha sehemu ndogo tu ya Watanzania. Hivyo  Vina uhalali wa kushiriki kama wadau wengine , asasi au mashirika mengine: kwa maoni yangu Vyingi haviongozwi na misingi ya demokrasia( internal democracy) Mimi najiuliza    kwanini Asili Mia tisini ya vyama tangu viundwe hadi Leo vinaongozwa na watu walewale tena wanaume 🀷🏽‍♂️Ni vyama vingapi vimefungua milango ya demokrasia shirikishi? Kwenye uongozi?? Kwangu mimi kuwe na tume huru ya kuongoza mchakato ili dhamira ya Rais wetu ya kuleta mabadiliko katika mifumo kandamizi na ya ubaguzi.


πŸ‘†πŸ‘†πŸ‘†πŸ‘†πŸ‘†Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na Tume ya Warioba.

[15:08, 11/05/2023] M:

 MTAZAMO WANGU: 

1. Napongeza Mwanzilishi wa Jukwaa hili kwa maana litasaidia kupata mawazo mapya; mbadala; kujikumbusha tulikotoka, tulipo na tunakokwenda ni wapi kuhusiana na suala la Katiba.


2. Mimi ninavyojua ni kwamba, Mchakato kuhusu mwendelezo wa Mabadiliko ya Katiba mpya ya Tanzania "Bado haujaanza rasmi katika kuuendeleza."  Kwa sababu:-


2.1: Tangazo la Serikali bado halijatolewa tena kuhalisha Mwendelezo wa Mchakato.


2.2: Bado hakuna na haupo Mwongozo wowote juu Mwendelezo wa suala hili maana siku zimepita nyingi saana tangu kukoma kwa Mchakato wa Katiba na Tangazo la Serikali likatoka juu ya kukoma kwake.

2.3: Tangu kukoma kwake, imepita takriban miaka 9 (hii ni miaka mingi) ambayo inatutaka kama taifa pengine Mchakato uanze upya ama uwe na mwendel…


[15:09, 11/05/2023] P: 

Naelewa mno ndio maana naona this is yet another waste of the Tanzanian people's time and tax money.


It's time tuwaheshimu watanzania na kuwaona wana akili timamu. Wanajua kinachoendelea wa sehemu kubwa tusema hawana tabia a ku protest kwa kila kitu.


Why these gimmicks every now and then?


The country has a lot of more pressing issues to deal with than keep tip toeing around Katiba Mpya wakati tunajua kinachoweza kufanywa na tunaweza kukifanya without all these back and forth drama.


[15:11, 11/05/2023] M:

 Mimi nadhani kazi kubwa ilifanyika chini ya Tume ya Warioba. Jambo la kuangalia tulikwama wapi na nini kifanyike kukwamua mchakato huu. Kwa wale wenye muda, tuipitie Rasimu hii na kutoa maoni yetu.


[15:15, 11/05/2023] T: 

Wazo la kujadili pamoja kwa staha ni jema.. na ndio maana mijadala hii ipo tumeanza na namna tunaovyona Msajili na majukumu yake anatakiwa atupitishe wapi Mjadala huu unaendelea na tutafika kote wajumbe wanakotaka tupite na uzuri wadau wote wako hapa..nashauri Lugha za staha na kuepuka mihemko ili tuwe na mawazo yenyetija kwa mustakabali wa pamoja...


[15:26, 11/05/2023] Pasta Martin: Precisely!


Tume ya Warioba walifanya kile ambacho hakijawahi kufanyika katika historia ya nchi hii nzuri. 


Kwa mara ya kwanza maoni ya wananchi yalikuwa broadly collected and accurately documented.


Tunajua wananchi (wenye nchi yao) walichotaka. Tatizo hatujawahi kuwa na utamaduni wa kuheshimu wanachotaka wananchi!


Demokrasia yetu ni ya kijanja janja hivi. Hata pale tunapojua wananchi wanataka nini lazima tu edit kidogo ili kuingiza matakwa yetu binafsi.


Even on this attaempt, we are commiting the same sin of arm twisting the public to bend to our tune.


Mchakato ulishaisha. Msimamizi wa mchakato bado yupo hai. Mzee Warioba bado yupo timamu kabisa. Kama nia yetu kweli ni kuheshimu maoni ya watanzania, kwa nini asiitwe msimamizi wa ukusanyaji wa maoni pek…


[15:31, 11/05/2023] M:

 MTAZAMO WANGU 2:

1. Msajili wa Vyama vya Siasa yuko chini ya Mamlaka katika Mhimiri mtambuka. Kwa hiyo, sio Mhusika Mkuu wa kuuendeleza Mchakato wa Mabadiliko ya Katiba mpya ya Tanzania.

2. Ninavyojua Mwendelezo wa suala hili liko chini ya "Wizara ya Sheria na Katiba" ndo wanaotakiwa kutoa Mwendelezo na Kutuongoza tunaanzaje na tunaendaje.

3. Kiongozi wa Jukwaa letu hili, ajikite katika kushinikiza Mwendelezo na uhalalishaji wa Mchakato husika.


[16:21, 11/05/2023] M: 

MTAZAMO WANGU 3:

1. Hoja/Mada ya kwanza iwe KUJIKUMBUSHA KUHUSU, "Mabadiliko ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mchakato ulianzaje, Ulifanyikaje na Uliishia wapi!?.":-


1.1: Kwa nini Wananchi walidai Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.?


1.2: Je, Wananchi na wadau mbalimbali walishiriki kikamilifu kutoa Maoni yao!?


1.3: Bunge la Katiba lilifanya kazi yake ipasavyo kuwakilisha makundi ya Jamii yote ya Tanzania kuipata Katiba waitakayo.?


1.4: Nini kilikwamisha kutokuwepo Katiba Mpya licha ya Mchakato kufanyika na ushiriki wa Wadau wa makundi yote kushiriki!?


2. Hoja/Mada ya pili iwe NAFASI NA WAJIBU WA SERIKALI KATIKA KUUENDELEZA MCHAKATO WA MABADILIKO YA KATIBA MPYA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA:-


2.1: Kwa sasa Serikali ifanye n…

[16:25, 11/05/2023] A: 

Naona sijajibiwa hoja yangu ipasavyo, pengine tujuzane  tu Hali ya sasa na  takwimu za sasa juu ya uelewa wa Mtanzania kuhusu maswala ya katiba Tanzania ikoje maana naona kama kuna mkanganyiko baina ya  wanaojua na sisi tusiojua..


[16:40, 11/05/2023] K: 

Mimi Sijaweza kupata takwimu kamili za hivi karibuni juu ya uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya katiba nchini Tanzania. Hata hivyo, ripoti mbalimbali zinaonesha kuwa uelewa wa wananchi kuhusu masuala ya katiba ni mdogo. Ripoti ya Jukwaa la Katiba Tanzania iliyochapishwa mwaka 2019 inaonesha kuwa asilimia 62 ya wananchi hawajui kuhusu mchakato wa katiba mpya nchini Tanzania.

Ripoti nyingine ya Taasisi ya Utafiti wa Sera za Kiuchumi na Kijamii (ESRF) ya mwaka 2018 inaonesha kuwa asilimia 50.8 ya wananchi hawaelewi kikamilifu maudhui ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Ripoti hiyo inaeleza kuwa wananchi wengi hawajui wajibu na majukumu ya serikali na wananchi, haki za msingi za binadamu, utawala bora na demokrasia.

Hata hivyo Rais wa Jamhuri Muungano wa Tanzania Mh. Dkt Samia Suluhu Hassan , amesiskika mara kwa mara akizitaka Taasisi za Kiraia na zile za kidini wasaidie katika kutoa elimu ya uraia katika katika maeneo haya, na wengine waliopewa majukumu naamini kabisa kuwa moderator umewaweka humu.

Ni muhimu sasa kwa serikali, asasi za kiraia, vyombo vya habari, na taasisi nyingine kushirikiana katika kutoa elimu na kuongeza uelewa kuhusu masuala ya katiba na mchakato wa kupata katiba mpya nchini Tanzania. Hii itasaidia kujenga uelewa wa pamoja kwa wananchi na kuongeza ushiriki wao katika mchakato huu muhimu wa kitaifa.


[16:41, 11/05/2023] K: 

Ninaunga Mkono Hii Hoja ni sawa sana!!


[16:44, 11/05/2023] K: 

1. Hoja/Mada ya kwanza iwe KUJIKUMBUSHA KUHUSU, "Mabadiliko ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mchakato ulianzaje, Ulifanyikaje na Uliishia wapi!?.":-

[16:45, 11/05/2023] Pasta Martin: This is a non-issue guys.


Watanzania wengi au wachache kujua Katiba au kutojua haizuwii au kusababisha chochote kifanyike au kisifanyike.


Kuna mambo mengi tu watanzania hawajui na yanafanyika lkn hakuna tatizo. 


Kwa Katiba, watanzania wanajua sana tu. Na walitoa maoni yao. Sasa hiyo kusema hawana uelewa inatoka wapi. Mi naona wasioelewa au wanaojifanya hawaelewi ni sisi wasomi na wajanja wachache tunaojadiliana humu kwenye mitandao.


[16:49, 11/05/2023] K: 

Hoja hii ya uelewa wa wananchi imetokana na ripoti za Utafiti na nadhani wasomi wanatembea na hizi takwimu ….ndicho kinachotatarajiwa kutoka kwa wasomi


[16:49, 11/05/2023] M: 

Mimi nadhani suala la Katiba kwa mwanchi wa kawaida, kwake is not an issue. Yeye anachohitaji ni utawala bora unaokidhi haki na huduma zake muhimu za kijamii. Zinapatikana vipi sio tatizo kwake. Hapo ndipo linapokuja suala la uwakilishi kupitia kwa wale wanaolewa nini maana ya Katiba ambayo ni sheria mama. Hivi niulize tu ni wangapi kati yetu siku za nyuma tumewahi kuhangaika kutafuta Katiba yetu inasemaje juu ya mambo mbali mbali? Ni kiri mimi sio miongoni mwa wale ambao nimewahi kujighulisha sana kujua vifungu vya Katiba yetu vinasemaje. Na kwa hali hiyo, sishangai sana watu kutoijua Katiba. Kama iliyopo mtu huijui utasumbuka kweli ni hiyo inayopiganiwa!!! Tuelezane ukweli tu kwamba Katiba ni eneo moja la taaluma ya Kisheria. Hata kwenye mijadala ya aina hii tuntegemea wanasheria kushiriki na kutuongoza zaidi. Huu ndio ukweli wenyewe.



[16:52, 11/05/2023] M: 

MTAZAMO WANGU 4 KULINGANA NA ULIVYOULIZA:

1. Suala la utoaji wa Elimu kwa Raia kuhusiana na Mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lazima utolewe Mwongozo wa Elimu yenyewe, kwa sababu kama Mchakato/Mwongozo toka Serikalini haujaanza rasmi AZAKI na Taasisi mbalimbali zitatoa Elimu gani.!?


[16:52, 11/05/2023] +255: 

Na ndiyo maana tuna wana sheria, hao kazi yao ni kusoma na kuelewa katiba, sheria na kanuni. Sisi wananchi tunataka utawala bora unaofuata sheria, kwa upande wa wananchi awatakaa waielewe sheria tena hasa hii iliyoandikwa kwa kizungu. Mamlaka zinachoweza kufanya ni kutengeneza uelewa wa haki za watu hayo mengine tutakutana mahakamani😊

[16:53, 11/05/2023] K: exactly

[16:54, 11/05/2023] K: Elimu ya aina ya Elimu!

[16:54, 11/05/2023] M: πŸ‘

[16:54, 11/05/2023] M: πŸ‘πŸ‘πŸ‘

[17:02, 11/05/2023] : ipi sasa namna bora ya kutoa elimu ya katiba na mchakato ndio huu uko jikoni



[17:05, 11/05/2023] K: πŸ€”Kwa Kufikiri kwa sauti  NINACHOONA, Kutoa elimu ya Katiba kunapaswa kuwa endelevu na yenye kufikia watu wengi iwezekanavyo. Hapa ni baadhi ya njia bora za kutoa elimu ya Katiba:

1. Kutoa elimu ya Katiba katika shule: Elimu ya Katiba inapaswa kuanza mapema shuleni. Wanafunzi wanapaswa kufundishwa kuhusu maana na umuhimu wa Katiba na jinsi inavyoongoza nchi yetu.


2. Matumizi ya teknolojia: Matumizi ya teknolojia kama vile mitandao ya kijamii, redio, televisheni, na programu za simu yanaweza kutumika kwa kutoa elimu ya Katiba kwa watu wengi zaidi.


3. Kutoa mafunzo kwa wanasiasa: Wanasiasa wana jukumu la kuelimisha wananchi kuhusu Katiba. Hivyo, mafunzo yatolewe kwa wanasiasa kuhusu maudhui ya Katiba ili waweze kutoa elimu sahihi kwa wananchi wao.


4. Kutoa semina na mihadhara: Semina na mihadhara ya umma yanaweza kutoa fursa kwa wataalamu wa Katiba na wananchi kujadili masuala mbalimbali yanayohusiana na Katiba.


5. Kutoa machapisho na vifaa vya elimu: Vifaa vya elimu kama vile vipeperushi, machapisho, na vitabu vinaweza kusambazwa kwa wananchi kama njia ya kutoa elimu ya Katiba.


Kwa ujumla, njia bora ya kutoa elimu ya Katiba ni kutumia njia mbalimbali za mawasiliano ili kufikia watu wengi iwezekanavyo na kuifanya iwe ya kuvutia na inayoeleweka kwa wananchi wote


[17:09, 11/05/2023] M: 

MTAZAMO WANGU 5:

1. Niombe kiongozi/viongozi wa Jukwaa hili kutenga muda na saa maalumu ya kuchangia hoja (Mfano Jioni/Asubuhi/Usiku ya siku inayofuata ndio Hoja/Mada itachangiwa na Itatolewa kwa wote ili siku inayofuata kwa muda utakaowekwa kuchangia).


2. Napendekeza Hoja/Mada moja isizidi SAA 1.20.


3. Baada ya Hoja/Mada kujadiliwa, yatolewe Majumuisho na Maazimio.


[17:10, 11/05/2023] K: 

Ni Haki ya Rais kuwa ndiye 'custodian' wa mchakato huu kwa nia njema tu, kwa nafasi yake kama The Executive anatarajiwa kuwa ndiye mjibu maswali pindi mambo yakienda mrama ( of which hatuombi yatokee ) but, Asante Hon Judge kwa insight hii!!πŸ™ŒπŸ½

[17:11, 11/05/2023] M: πŸ‘πŸ‘πŸ‘

Safi

[17:12, 11/05/2023] T: Kunamambo ya kujifunza hapa safi sana..mchanganuo wenye tija


[17:15, 11/05/2023] +25: Kwani wanamlalamika bila kushauri? Muhimu tuangalie nini kinashauliwa kutoka kwako na sio kutaka watu Woote wasifie 

Me naona hata hao wasaidizi wake pia wanategemea mawazo yetu na taasisi inajua kutakua na lawama ushauri


[17:15, 11/05/2023] M: Mimi nafikiri katika mijadala itakayofuata na nadhani hata hii ambayo imekwisha anza, ijikite zaidi kutafuta sababu za kukwama kwa mchakato wa Katiba uliopita. Tukivuka ngazi hiyo kwa kuafikiana, then tatakuwa tumepiga hatua mbele ya kupata Katiba tunayoitaka.

[17:17, 11/05/2023] M: Safi..!πŸ‘


[17:36, 11/05/2023] +255: 

 kwa Kuzingatia Haya. kuwe na utaratibu mzuri wa kuwafikia viongozi wa serikali za mitaa(kata) na viongozi wa vyama vya siasa (kata) nchi nzima hapa ndio mzizi wa fitina wa kujua au kutoijua katiba kwa wananchi utakua ukomo wake na maoni yatapatikana hapa na kila kitu kama sheria zote ndogo au sheria za halmashuri zinavyoshirikishwa kwa wananchi na zinapelekwa bungeni na mwisho kufanya kazi hili muhimu sana.... ngazi ya chini ya serikali za mitaa na vyama vya siasa uko chini linatibu kila kitu...


[17:42, 11/05/2023] P: 

Kuna nchi nyingi tu duniani ambazo wananchi wake hawajui Katiba yao inasemaje, na hawajali. 


Lakini kutokana mifumo imara ya kiutawala na UZALENDO wa viongozi wao husikii watu wakipewa elimu ya Katiba. Ili iweje?


Sisi hata tukifundishana katiba tukatoa na mitihani  kabisa. Kama nia ya Katiba mpya haipo haipo tu.


Tutapeana elimu. Tupoteze muda. Tutatumi pesa. Lakini kama nia haipo, itabaki hivi hata miaka 10 ijayo.


[17:49, 11/05/2023] +: 

Jamani mimi ni mgeni humu ndani, tafadhali msinipige mawe..... Katika huu mchakato mpya wa katiba mpya,  ile katiba ya Warioba inawekwa wapi? Au inakuwa kama Research Report!?? Maana kama kumbukumbu zangu ziko sahihi ilikuwa karibu na stage ya adoption. Na kama inakuwa considered, je mchakato utapaswa kuanzia stage gani??


[17:51, 11/05/2023] Kopwe:

 ni vyema tusifike hapaπŸ‘†πŸΎ labda tunapishana namna nina Imani hata kama dhamiri haikuwepo sasa ipo tuanzie hapo! kwa kujenga juu ya "tofali hili"


[17:55, 11/05/2023] T: 

Nini sasa wajibu wa vyama vya siasa katika mchakato wa katika kwa sasa kunawano laumu na tukirudi nyuma hawa hawa wametufikisha hapa....


[18:10, 11/05/2023] K: 

Vyama vya siasa  jukumu lao ni kubwa sana katika mchakato wa katiba mpya nchini Tanzania kwa hapa tulipo. Ninaamini wana Wajibu wa kushiriki kikamilifu katika mchakato huu, kwanza kwa kutoa maoni yao kuhusu vipengele mbalimbali vya katiba mpya na Pili, kutoa mapendekezo yao kwa ajili ya kuboresha rasimu ya katiba.

Tunaweza kuona mifano ya wajibu wa vyama vya siasa katika mchakato wa katiba ambayo ni pamoja na;


1. Kutoa maoni yao kuhusu vipengele mbalimbali vya katiba: Vyama vya siasa vinapaswa kutoa maoni yao kuhusu vipengele mbalimbali vya katiba mpya, kama vile mfumo wa serikali, muundo wa bunge, muundo wa vyombo vya dola na masuala mengine yanayohusiana na demokrasia na utawala bora.


[18:15, 11/05/2023] K:

 2. Kuhamasisha wananchi kushiriki katika mchakato wa katiba: Vyama vya siasa vinaweza kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa katiba kwa kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa katiba mpya na kuwahimiza kutoa maoni yao kuhusu rasimu ya katiba.


3. Kutoa mapendekezo ya kuboresha rasimu ya katiba: Vyama vya siasa vinapaswa kutoa mapendekezo yao kwa ajili ya kuboresha rasimu ya katiba, kwa kuzingatia maslahi ya wananchi na mahitaji ya taifa kwa ujumla.


4. Kusimamia utawala bora na demokrasia: Vyama vya siasa vinapaswa kusimamia utawala bora na demokrasia kwa kuhakikisha kuwa mchakato wa katiba unafanyika kwa njia ya uwazi, ushirikishwaji wa wadau mbalimbali na kwa kuzingatia misingi ya demokrasia na utawala bora.

Kiukweli, vyama vya siasa vina jukumu muhimu katika kutoa maoni yao, kuhakikisha ushirikishwaji wa wananchi na kusimamia utawala bora na demokrasia.


[18:22, 11/05/2023] T: Karibu sana pamoja na kwamba swala hili liko Mbele lakini wataalamu hapa watakujibu kwa kifupi ili tuiweke kama MADA Baada ya kujadili wazo la @M "1. Hoja/Mada ya kwanza iwe KUJIKUMBUSHA KUHUSU, "Mabadiliko ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mchakato ulianzaje, Ulifanyikaje na Uliishia wapi!?.":-


[18:31, 11/05/2023] T:

 Nakumbuka Mwanasheria Nguli na mataalamu mambo ya katiba ambae pia ni Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu alisema  Namnukuu "mchakato wa Katiba Mpya lazima utungiwe Sheria mpya ,sheria iliyounda Tume ya Warioba na Bunge Maalum la Katiba haiwezi kutumika tena, sababu ilishakamilisha majukumu yake.

Hivyo, tutachukua baadhi ya mambo mazuri kwenye rasimu ya Warioba, tutachukua baadhi ya mambo kwenye Katiba pendekezwa na kuyaunganisha na mawazo mapya ya wananchi ili tupate Katiba Mpya iliyo bora."


Chanzo: ITV

Comments

Popular posts from this blog

Historia ya utawala wa Kijerumani katika eneo la Tanganyika inahusisha kipindi cha ukoloni wa Kijerumani ambacho kilidumu kati ya mwaka 1885 na 1916