HISTORIA FUPI YA MUUNDO WA KATIBA WAKATI WA WAKOLONI HADI SASA

 
Ilitufikie malengo ya kutambua na kuelewa kwanini Katiba ni muhimu katika Nchi, yapaswa tujue Historia Pana ya Katiba na Sheria zeta kabla na baada ya Ukoloni  fuatana nasi Hapa kutambua  Katiba ya Watu ni ipi hasa

Kwa ujumla nchi nyingi hasa zile zinazoendelea zina katiba zilizoandikwa.nyingi kati ya katiba hizo zilitungwa na kurekebishwa na watawala wa kikoloni, na nyingine zilitungwa baada ya makubaliano na tawala za kikoloni kabla ya kuondoka.Katiba hizo ni maridhiano ambayo yalilinda maslahi ya pande zote mbili:


(1)Tawala za kikoloni zilizokuwa zikiandika.
(2)Nchi iliyokuwa ikipata uhuru

"Katiba nyingi katika nchi zilizoendelea zina uhusiano na Katiba na Tawala za kikoloni.

Historia ya katiba hapa Tanzania pia ina uhusiano na tawala za kikoloni zilizokuwa zinatawala kabla ya uhuru 



Historia Ya Mabadiliko Ya Katiba Tanzania 1961 Katiba ya kwanza ya uhuru iliyowekwa na Waingereza (Independence Constitution).

Mwaka 1962 Katiba ya Jamhuri (The Republic Constitution) iliitambua Tanganyika kama Jamhuri na ilipunguza madaraka ya Bunge(Iliwekwa na Waingereza). 

Katiba Hiyo  iliruhusu mfumo wa vyama vingi, na Vyama vifuatavyo vilisajiliwa:TANU, United Tanganyika Party(UTP), African National Congress(ANC), The Peoples Democratic Party(PDP), Peoples Convertion Party(PNP), National Enterprise Party(NEP), All Muslim Nationalist Union of Tanganyika(AMNUT), African Independence Movement(AIM).

Lakini mwaka 1963 Halmashauri Kuu ya TANU ilipitisha maamuzi kufanya Tanganyika kuwa nchi ya chama kimoja.Ikafuatia mwaka 1965 Sheria ya chama kimoja iliingizwa kwenye Katiba 

Mwaka 1965 Iliwekwa katiba ya muda (The Interim Constitution) 

Mwaka 1977 Haki za binaadamu ziliingizwa rasmi katika Dibaji.Mwaka 1984 Katika katiba ya Jamhuri haki za binadamu ziliingizwa rasmi katika katiba.Mwaka1992 Katiba iliruhusu tena mfumo wa vyama vingi kwa shinikizo la nchi za kibeberu









Comments

Popular posts from this blog

UTARATIBU WA USAFI WA MAZINGIRA NAO UWEKWE KWENYE KATIBA?SWALI LA MDAU KWENYE FORUM YA KATIBA YA WATU

Historia ya Vita vya Majimaji inaonesha kuwa awali walikamatwa machifu 48 na baadaye kukamatwa wengine ambapo idadi ya machifu walionyongwa na kuzikwa katika kaburi moja ilifikia 66.

TATHMINI YA MJADALA KATIKA FORUM YA KATIBA YA WATU KUWEKA USAFI WA MAZINGIRA KAMA HAKI YA MSINGI KIKATIBA YA WATANZANIA