KATIBA YA NCHI NI NINI?

Katiba ya Nchi ni nini?
Katiba ya nchi ni muafaka wa kitaifa unaoanisha namna taifa linavyohitaji

kujitawala katika mambo yote na kuendesha mambo yake. Hivyo basi,
Katiba ya nchi ni sheria mama inayoainisha misingi mikuu ya kisiasa na
kuonyesha madaraka na majukumu ya serikali pia huanisha haki za msingi
za wananchi. Katiba ya nchi hutungwa na wananchi wenyewe kama
watu huru ili kupata muafaka wa taifa lao na namna gani wangependa kujitawala.


Kwa kifupi, Katiba sio chombo cha wanazuoni wachache bali ni chombo
kinachoonyosha umiliki wa nchi na rasilimali ya wananchi, nafasi ya 3
wananchi katika utawala na namna gani wangependa kuweka utawala
wa nchi yao na hivyo kutengeneza muundo wa serikali yao.

Kwa hiyo

Katiba ya nchi ni waraka wa kitaifa unaoweka bayana, pamoja na
mambo mengine, mfumo wa haki za msingi kwa wananchi wake,
mihimili yake ya dola, namna ya kuweka utawala katika ngazi
zote, muundo wa serikali yao na namna ya usimamizi wa mapata
na matumizi ya rasilimali yote ya kitaifa bila ukandamizaji wa aina
yeyote kwa jinsia zote




 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTARATIBU WA USAFI WA MAZINGIRA NAO UWEKWE KWENYE KATIBA?SWALI LA MDAU KWENYE FORUM YA KATIBA YA WATU

Historia ya Vita vya Majimaji inaonesha kuwa awali walikamatwa machifu 48 na baadaye kukamatwa wengine ambapo idadi ya machifu walionyongwa na kuzikwa katika kaburi moja ilifikia 66.

Mjadala kuhusu umuhimu wa elimu ya Katiba na uelewa wa sheria kwa wananchi unajumuisha masuala muhimu yanayohusu ujenzi wa demokrasia, utawala bora, na usawa katika jamii. Hapa kuna taarifa na tathmini ya kina juu ya mjadala huo: