KATIBA ni sheria au kanuni zinazoainisha jinsi ambavyo nchi, chama, au shirika vitakavyoendesha shuguli zao.
KWA UPANDE WA WANANCHI, katiba ni sheria mama inayoainisha misingi mikuu ya kisiasa na kuonyesha madaraka na majukumu ya serikali. Katiba za nchi pia huainisha haki za msingi za wananchi.
Kuna aina kuu mbili za Katiba
(a) Katiba isiyo ya maandishi (ya kimapokeo)
(b) Katiba ya maandishi.
MKUTANO WA WADAU WA DEMOKRASIA KUJADILI MASUALA MAHSUSI YA ZANZIBAR
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Demokrasia ni nini? Demokrasia ni mfumo wa serikali ambapo wananchi wote ni sawa mbele ya sheria na wanashiriki katika kufanya maamuzi ya kitaifa juu ya masuala ya Umma. Wakati mwingine wananchi hushiriki moja kwa moja - hii ina maana kwamba wao hupiga kura moja kwa moja kwenye masuala kama vile sheria na katika chaguzi. Wakati mwingine huwakilishwa na viongozi wao waliowachagua. Ni utawala wa watu, na watawala hutawala kwa ridhaa ya watu. Kwa hiyo kwa kifupi Demokrasia ni mfumo unatoa fursa ya madaraka kwa Umma moja kwa moja au kutokana na uwakilishi. Abraham Lincoln, Rais wa 16 wa Marekani, alisema Demokrasia ni serikali ya watu/mfumo wa utawala wa watu, kwa ajili ya watu na unaotokana na watu. Watu wanaunda serikali.
Aina za demokrasia
1. Demokrasia ya moja kwa moja (kwa Kiingereza "Direct Democracy") ni aina ya demokrasia ambayo wananchi wote wanaweza kushiriki katika kuamua masuala ya kisiasa, ya kijamii, ya kisheria na ya kiuchumi bila kutumia chombo cha uwakilishi kama vile bunge. Uwezo huu wa wananchi kutoa maamuzi unaweza kuwapa hata uwezo wa kimahakama, ingawa mara nyingi wananchi hupewa uwezo wa kutunga au kupitisha sheria tu.
Demokrasia ya moja kwa moja ni tofauti na demokrasia inayofuatwa katika nchi nyingi duniani hivi sasa, ambapo wananchi huchagua wawakilishi wao katika uchaguzi. Nchi ya Uswisi ni maarufu kwa mfumo wake wa demokrasia ya moja kwa moja ambako sheria nyingi zinaamuliwa na wananchi wote kwa njia ya kura. 2. Demokrasia shirikishi ("Representative Democracy"): hapo wachache hupewa na wengi dhamana katika uwakilishi wa jamii katika maamuzi. Wachache huchaguliwa na wengi kwa njia ya demokrasia huru na ya haki kwa kufuata Katiba ya nchi hiyo. Mfano: Wabunge huwakilisha wananchi wao katika kuleta maendeleo na kuishauri serikali juu ya maendeleo ya nchi yao. Misingi ya demokrasia
·Uwepo wa vipindi vya uchaguzi wa viongozi na chaguzi zenye kuzingatia haki na usawa.
·Kuwepo uchaguzi huru na uwanja sawa wa kisiasa.
·Wananchi wawe na fursa kikatiba kupata taarifa, vyanzo vya taarifa viwepo na kulindwa kisheria.
·Wananchi na wanajamii wawe na fursa ya kuunda vyombo vya kijamii mathalani asasi za kiraia.
·Kuwa na taasisi zinazolinda na kuchochea ustawi wa demokrasia nchini.
Umuhimu wa demokrasia
·Kukosoa matumizi mabaya ya fedha na viongozi kwa misingi ya demokrasia.
·Kushirikishwa kupanga kusimamia miradi ya maendeleo katika maeneo yao.
·Kuunga mkono jitihada za serikali katika kuchochea ustawi na maendeleo kwa jamii.
·Kuhoji utendaji wa serikali kuanzia ngazi ya mtaa, kata, kijiji, wilaya kuhakikisha uwazi, uadilifu na uwajibikaji.
Faida za demokrasia
·Matumizi mazuri ya rasilimali za nchi.
·Maendeleo endelevu.
·Kupungua kwa umasikini, ujinga na maradhi.
·Kutokomea kwa rushwa.
·Huduma bora za jamii.
·Amani na utulivu.
·Kuheshimiwa kwa haki za binadamu.
·Utatuzi wa migogoro kwa mujibu wa sheria na taratibu.
·Kuleta ustawi wa wananchi.
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Comments
Popular posts from this blog
-
TAHMINI YA KINA, USHAURI NA MAPENDEKEZO KUHUSU MJADALA WA WARAKA WA TEC KATIKA FORUM YA KATIBA YA WATU 1. UTANGULIZI WA MJADALA Mnamo tarehe 22 Juni hadi 23 Juni 2025 , Forum ya Katiba ya Watu iliendesha mjadala wa kina kuhusu waraka wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC) unaohusu maboresho ya maadhimisho ya kiliturujia — hususan kupiga marufuku hotuba zisizo za kiliturujia ndani ya ibada, zikiwemo za viongozi wa kisiasa au kijamii. Mjadala huo uliwashirikisha washiriki 1,023 wakiwemo wanazuoni wa katiba, wanaharakati, viongozi wa dini, na wananchi wa kawaida. Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, mjadala huu unahusu uhuru wa dini (Ibara ya 19) , haki ya kuabudu, mipaka ya kisiasa katika maeneo ya ibada, na tafsiri ya heshima kwa viongozi wa serikali katika majukwaa ya kidini 2. TAHMINI YA MJADALA: MTAZAMO WA KISHERIA, KIDINI NA KIJAMII 2.1 Muktadha wa Kikatiba Ibara ya 19 ya Katiba ...
MJADALA JUU YA WALAKA WA KANISA KATOLIKI JUU YA KATAZO LA MATANGAZO AMA SALAMU WAKATI WA IBADA KATIKA FORUM YA KATIBA YA WATU Mdau @alianza kwa kutoa taarifa hii iliyochapishwa na jamii Forum MAJIBU YA WADAU [22/06/2025, 18:50:13] Tan: Taarifa hiyo ya Kanisa Katoliki kuhusu maboresho ya maadhimisho ya kiliturujia inaweza kuelezwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kama ifuatavyo: 1. Uhuru wa Dini (Ibara ya 19) Katiba ya Tanzania, Ibara ya 19, inatambua na kulinda uhuru wa kuabudu na uhuru wa mtu kuendesha shughuli za kidini kwa mujibu wa imani yake, ilimradi hazikiuki sheria za nchi: “Kila mtu anayo haki ya uhuru wa mawazo, imani na dhamira, pamoja na uhuru wa dini.” Kwa msingi huu, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) lina mamlaka ya kupanga na kusimamia namna ibada zao za kiliturujia zinafanyika, ikiwa ni pamoja na kuweka masharti au mabadiliko ndani ya maadhimisho kama ndoa, daraja takatifu, maziko, nadhiri za kitawa, n.k....
Makumbusho ya Taifa ya Majimaji ni eneo ambalo limehifadhiwa vizuri na serikali ili kuwawezesha watu kujifunza kumbukumbu nyingi ambazo ni kivutio adimu cha utalii wa kishujaa na kiutamaduni. Watu kutoka mkoa wa Ruvuma na nje ya nchi wanatembelea eneo hili maarufu katika historia ya Tanzania hasa katika harakati ambazo zilifanywa na babu zetu kupambana na wakoloni ili kujitawala wenyewe bila kunyonywa. Mkurugenzi wa makumbusho ya Taifa ya Majimaji mhifadhi Kiongozi Balthazar Nyamusya anasema eneo hilo la makumbusho lina historia tatu ambazo ni historia ya vita vya majimaji,historia ya ujio wa wangoni kutoka Afrika ya Kusini na historia ya uhuru wa Tanganyika. Anaitaja historia ya vita vya majimaji ililenga kumkomboa mtanzania kutoka mikononi mwa wakoloni Wajerumani na kwamba sio sahihi kuwa vita hiyo ilikuwa na uwezo wa kugeuza risasi kuwa maji bali ililenga kuwapa nguvu wapiganaji kujitolea hata ikibidi kupot...
Comments
Post a Comment