KATIBA ni sheria au kanuni zinazoainisha jinsi ambavyo nchi, chama, au shirika vitakavyoendesha shuguli zao.
KWA UPANDE WA WANANCHI, katiba ni sheria mama inayoainisha misingi mikuu ya kisiasa na kuonyesha madaraka na majukumu ya serikali. Katiba za nchi pia huainisha haki za msingi za wananchi.
Kuna aina kuu mbili za Katiba
(a) Katiba isiyo ya maandishi (ya kimapokeo)
(b) Katiba ya maandishi.
MKUTANO WA WADAU WA DEMOKRASIA KUJADILI MASUALA MAHSUSI YA ZANZIBAR
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Demokrasia ni nini? Demokrasia ni mfumo wa serikali ambapo wananchi wote ni sawa mbele ya sheria na wanashiriki katika kufanya maamuzi ya kitaifa juu ya masuala ya Umma. Wakati mwingine wananchi hushiriki moja kwa moja - hii ina maana kwamba wao hupiga kura moja kwa moja kwenye masuala kama vile sheria na katika chaguzi. Wakati mwingine huwakilishwa na viongozi wao waliowachagua. Ni utawala wa watu, na watawala hutawala kwa ridhaa ya watu. Kwa hiyo kwa kifupi Demokrasia ni mfumo unatoa fursa ya madaraka kwa Umma moja kwa moja au kutokana na uwakilishi. Abraham Lincoln, Rais wa 16 wa Marekani, alisema Demokrasia ni serikali ya watu/mfumo wa utawala wa watu, kwa ajili ya watu na unaotokana na watu. Watu wanaunda serikali.
Aina za demokrasia
1. Demokrasia ya moja kwa moja (kwa Kiingereza "Direct Democracy") ni aina ya demokrasia ambayo wananchi wote wanaweza kushiriki katika kuamua masuala ya kisiasa, ya kijamii, ya kisheria na ya kiuchumi bila kutumia chombo cha uwakilishi kama vile bunge. Uwezo huu wa wananchi kutoa maamuzi unaweza kuwapa hata uwezo wa kimahakama, ingawa mara nyingi wananchi hupewa uwezo wa kutunga au kupitisha sheria tu.
Demokrasia ya moja kwa moja ni tofauti na demokrasia inayofuatwa katika nchi nyingi duniani hivi sasa, ambapo wananchi huchagua wawakilishi wao katika uchaguzi. Nchi ya Uswisi ni maarufu kwa mfumo wake wa demokrasia ya moja kwa moja ambako sheria nyingi zinaamuliwa na wananchi wote kwa njia ya kura. 2. Demokrasia shirikishi ("Representative Democracy"): hapo wachache hupewa na wengi dhamana katika uwakilishi wa jamii katika maamuzi. Wachache huchaguliwa na wengi kwa njia ya demokrasia huru na ya haki kwa kufuata Katiba ya nchi hiyo. Mfano: Wabunge huwakilisha wananchi wao katika kuleta maendeleo na kuishauri serikali juu ya maendeleo ya nchi yao. Misingi ya demokrasia
·Uwepo wa vipindi vya uchaguzi wa viongozi na chaguzi zenye kuzingatia haki na usawa.
·Kuwepo uchaguzi huru na uwanja sawa wa kisiasa.
·Wananchi wawe na fursa kikatiba kupata taarifa, vyanzo vya taarifa viwepo na kulindwa kisheria.
·Wananchi na wanajamii wawe na fursa ya kuunda vyombo vya kijamii mathalani asasi za kiraia.
·Kuwa na taasisi zinazolinda na kuchochea ustawi wa demokrasia nchini.
Umuhimu wa demokrasia
·Kukosoa matumizi mabaya ya fedha na viongozi kwa misingi ya demokrasia.
·Kushirikishwa kupanga kusimamia miradi ya maendeleo katika maeneo yao.
·Kuunga mkono jitihada za serikali katika kuchochea ustawi na maendeleo kwa jamii.
·Kuhoji utendaji wa serikali kuanzia ngazi ya mtaa, kata, kijiji, wilaya kuhakikisha uwazi, uadilifu na uwajibikaji.
Faida za demokrasia
·Matumizi mazuri ya rasilimali za nchi.
·Maendeleo endelevu.
·Kupungua kwa umasikini, ujinga na maradhi.
·Kutokomea kwa rushwa.
·Huduma bora za jamii.
·Amani na utulivu.
·Kuheshimiwa kwa haki za binadamu.
·Utatuzi wa migogoro kwa mujibu wa sheria na taratibu.
·Kuleta ustawi wa wananchi.
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Comments
Popular posts from this blog
-
Watalaam wa Sheria kutoka Urusi Wawasili Tanzania Kuelimisha Kuhusu Mapambano dhidi ya Uhalifu wa Kimataifa Kongamano hili la kitaaluma linalowajumuisha watalaam wa sheria kutoka Urusi ni hatua muhimu katika kukuza uwezo wa taaluma ya sheria na kupambana na uhalifu wa kimataifa nchini Tanzania. Kuwasiliana na kushirikiana na wataalamu wa sheria kutoka nchi nyingine ni muhimu sana katika ulimwengu wa leo unaovuka mipaka. Kongamano hili linatoa fursa kwa wataalamu wa sheria wa Tanzania kujifunza kutokana na uzoefu na mbinu za kupambana na uhalifu wa kimataifa kutoka kwa wenzao wa Urusi. Kuongeza Uwezo wa Kitaaluma Kwa kushiriki katika kongamano hili, wanasheria wa Tanzania wanaweza kupata ufahamu mpana kuhusu mifumo na mikakati ya kisheria inayotumiwa na wenzao wa Urusi katika kupambana na uhalifu wa kimataifa. Hii inaweza kusaidia kuboresha uwezo wa kitaaluma wa wanasheria wa Tanzania na kuongeza ufanisi katika kushughulikia masuala ya kisheria ya kimataifa. Ush...
Kabla ya Uingereza kuchukua udhibiti wa eneo hilo wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Kipindi hiki kilikuwa sehemu ya jumla ya eneo la Afrika Mashariki ya Kijerumani, ambalo liliundwa na makubaliano ya kimataifa ya Mkutano wa Berlin wa 1884-1885. Sheria na utawala wa Kijerumani ulileta mabadiliko kadhaa katika Tanganyika, na mifumo ya kijadi iliyokuwepo ikashughulikiwa kwa njia ambazo zilikuwa na athari kubwa kwa jamii za Kiafrika. Baadhi ya vipengele muhimu vya utawala wa Kijerumani na mifumo ya sheria ni kama ifuatavyo: Mifumo ya Utawala: Wajerumani walijaribu kuanzisha utawala wa kikoloni na kuleta mfumo wa utawala wa kisheria uliounganisha na utawala wa Kiingereza na Kifaransa katika makoloni mengine ya Afrika. Utawala wa Kijerumani ulizingatia utawala wa moja kwa moja na kuweka nguvu kubwa mikononi mwa maafisa wa Kijerumani walioteuliwa. Mabadiliko katika Mifumo ya Ardhi: Wajerumani walijaribu kuanzisha mfumo wa umiliki wa ardhi wa Kizungu, ambapo ardhi iligawanywa na kugawiwa ...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal 2 Jijini Dar es Salaam tarehe 23 Oktoba, 2022. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo wakati wa Wimbo wa Taifa wa Tanzania ukipigwa mara baada ya Rais huyo wa DRC kuwasili nchini tarehe 23 Oktoba, 2022. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mhe. Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo wakati wakiangalia vikundi mbalimbali vya ngoma za asili vikitumbuiza mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal 2 Jijini Dar es Salaam tare...
Comments
Post a Comment