MKUTANO MAALUM WA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA   NCHINI, UKIJADILI   NA KUPOKEA MAONI YA MSWADA WA SHERIA ZA   UCHAGUZI NA SHERIA ZA VYAMA VYA SIASA. 

Baraza la Vyama vya Siasa nchini liliandaa Mkutano Maalum wa kujadili na kupokea maoni ya Wadau juu ya mswada wa Sheria za Uchaguzi na Sheria za Vyama vya Siasa ambayo ni matokeo ya mapendekezo ya Kikosi Kazi kilichoundwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.


Mgeni Rasmi katika mkutano huu alikuwa Bw. Othman Masoud Othman, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Wadau na Washiriki walijulishwa na kuhusu lengo la Mkutano, pamoja na mambo mengine, ilielezwa kuwa ni Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa utakaojadili na kupokea maoni ya mswada wa Sheria za Uchaguzi na Sheria za Vyama vya Siasa 


Kauli mbiu ya mkutano huu Ilikuwa ni “Toa Maoni Yako Kuimarisha Demokrasia”. Mara baada ya maelezo haya. Mkutano huu uliratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu kwa kushirikiana Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Katika ufunguzi wa mkutano huu taratibu zote na itifika ilizingatiwa ipasavyo na kikao kilifunguliwa rasmi na Mgeni Rasmi.


ITAENDELEA.......

Comments

Popular posts from this blog